Mchango
wa Waislamu Katika Maendeleo ya Dunia
na Hamza Z. Rijal
Katika makala iliopita ikiwa ni utangulizi wa
maudhui ya Mchango wa Waislmau katika maendeleo ya dunia nilijaribu kutoa
ufafanuzi kuwa Waislmau sivyo wanavyoonekana na kunasibishwa na ugaidi lakini
Waislamu wameweza kutoa michango mikubwa ya kuifanikisha dunia hii tunayoishi
kuwa katika maendeleo na mafanikio.
Kati ya vigogo mbalimbali wa Kiislamu ambao
wamefanya kazi kubwa ambao wataelezewa katika mfululizo wa makala hizi ni
pamoja na : Muhammad Ibn Musa Al-Khwarizm (780 – 850), Ibn Battuta (1304 –
1369), Ibn Rushd (1126 – 1198), Omar Khayyam (1048 – 1131), Thabit Ibn Qurra
(826 – 901), Abu Bakr Al-Razi (865 – 925), Jabir Ibn Haiyan (722 – 804), Ibn
Ishaq Al-Kindi (801 – 873), Ibn Al-Haytham (965 – 1040), Ibn Zuhr (1091 –
1161), Ibn Khaldun (1332 – 1406), Ibn Al-Baitar (1197 – 1248), Abu nasr
Al-Farabi (872 – 950), Al-BattanI (858 – 929), Ibn Sina (980 – 1037).
Msomi Al-Khwarizmi
Mjuwe
Muhammad Ibn Musa Al-Khwarizm (780 – 850)
Muhammad
ibn Mussa Al-Khawarizimi ni Mfursi aliobobea katika fani nyingi za kitaluma
ikiwa Hesabati, Elimu ya nyota, Jiografia na elimu nyenginezo, hizo
nilizokwisha kuzinukulu ndizo alizozifanyia kazi kwa kiwango kikubwa.
Al-Khawarizimi
amezaliwa huko Uajemi katika mwaka wa 780AD. Katika historia tunamsoma Kiongozi
Haroun Rashid ambaye katika uongozi wake aliusukuma na kupeleka Uislamu mbele
katika fani ya elimu na ndio nyakati hizo zikijulikana kama nyakati za dhahabu
kumanisha kuwa ninyakati ambapo Waislamu walifanikiwa na kutekeleza mengi
katika elimu na maendeleo au kwa kifupi tunaweza kuita ni wakati wa mafanikio
na maendeleo makubwa. Kujulikana kwa Al-Khawarizimi na kuweza kufanya kazi zake
kwa upana ni pale alipokuwa Baghdad katika Nyumba ya Hekima (house of wisdom)
chini ya Kiongozi al-Mamun huyu akiwa ni mwana wa Kiongozi Haroun Rashid.
Kubakia
kwake Baghdad Al-Khawarizimi aliweza kuja na nadharia mbalimbali za hesabati na
ufanyaji wa hesabu kwa njia rahis kabisa kwa kutumia Logarithm inaeleweka kuwa alibobea mno katika fani hii ya Algorithm ambayo fani hii ndio
inayotumika katika Computer kuwezesha kufanya kazi kwa kirahisi. Baadhi ya
wasomi hupenda kumwita Al-Khawarizimi kuwa ni babu wa somo la Computer kwa kuwa
dhana nzima inayotumika katika Compure mizizi yake imetokana nayeye.
Juu ya kazi kubwa iliofanywana Al-Jabir katika
somo la Algebra lakini Al-Khawarizimi
naye amefanya kazi kubwa ndani ya fani hii hasa unaposoma kitabu kinachojulikana
Hisab al-Jabr wa-al-Muqabala. Kitabu
hiki katika taaluma ya sayansi kilibidi kufasiriwa mara mbili kwa lugha ya Kilatino
lugha ambayo huko nyuma ikijulikana kama ni lugha ya taaluma. Walikuwa Gerard
wa Cremona na Robert wa Chester katika
karne ya 12 walipoifanyia tafsiri kazi yake hiyo ya Hisab al-Jabr wa-al-Muqabala.
Al-Khwarizm aliidhibiti taaluma ya utambuzi wa
hesabu zijulikanazo kama Quadratic
equations ambazo alitoa mifano zaidi ya 100 katika kuweza kupata jawabu
unapofanya Quadratic equations aidha aliweza kufahamisha somo la Geometry na kuweka mifano mbalimbali ya
kuweza kulielewa somo hilo. Fani hizi mbili ambazo nimezielezea, aliweza
kurahisisha kugawa mirathi kwa njia ya kirahisi kabisa kwa kutumia Quadratic equations na mifano yake ya
Geometry ndio yalioleta chimbuko la upimaji wa ardhi ambao hadi hii leo njia
alizozipita ndizo zinazotumika.
Bahati mbaya katika taaluma tunazozisoma jina
lake huwa haliguswi kwa uchoyo wa nchi za Magharibi uchoyo huu sio kwa Waislamu
tu bali hata watu wa jamii nyengine waliokuwa sio Waislamu walifanyiwa uchoyo
huo, kwa mfano V. N. Sukachov katika mwaka wa 1910 huyo akiwa ni Mrusi ni mtu
wa mwanzo ambaye alielezea kuwa kila kiumbe kina mwahali pake anaposihi na hapo
ndipo panakuwa na maingiliano ya maisha na mazingira yaliokizunguka kiumbe
hicho nadharia ya kisomi inajulikana kama Ecosystem,
akiwa Sukachev alioasisi neno hilo na kuwa anayasomesha na kuyaelezea katika
vyuo vya Urusi nchi za magharibi hawana habari au waliibeza kazi hii mpaka
alipokuja A. G. Tansley mwaka wa 1935 na kuielezea suala zima la ecosystem na kubatizwa kuwa Tansley ni
muanzilishi wa dhana nzima ya ecosystem,
na katika makala hizi utaona msomaji kuwa hata yale majina yao wataalamu hawa
wa Kiislamu yanaojitambulisha kuwa ni watu wa maeneo gani yamebadilishwa na
kufanywa majina yao yatamkwe kizungu, mfano Al-Khawarizimi anatamkwa kama Algoritmi au Algaurizin
Al-Khwarizmi amefanya kazi kubwa katika elimu
ya nyota na kuandaa kalenda, kufanya hesabu na kujua kwa dhati sehemu ya jua mwezi
na sayari zinapokuwa huyu ndio muasisi
wa table kwa wasomi wa hesabu za sine na tangents. Katika kitabu
chake cha Zij al- sindhind ambacho kimejikita katika elimu ya nyota, Al-Khawarizimi
alichukua rejea nyingi tu kutoka Uhindini na kwengineko kuweza kukifanikisha
kitabu chake.
Al-Khawarizmi akiwa amefanya hesabu kwa njia ya
Alogarithm miaka 200 iliopita hii leo ndio taaluma hii inatumika kwa kiwango
kikubwa, ni yeye Al-Khawarizimi alizozijulisha nambari za kiarabu kutumika
katika nchi za Magharibi na kuifanya Zero nayo itumike katika kujumuisha ingawa
wengi wanasema kuwa Zero iliasisiwa katika Bara la Uhindi na Al-Khawarizimi
alisoma maandiko mengi ya Uhindini lakini kujulikna kwa Zero huko Ulaya
inatokana na maandiko yake Al-Khawarizimi.
Al-Khawarizimi amefanya kazi nzito katika somo
la Jiografia, pale aliporekebisha kazi ya Ptolemy
ya utafiti wa Jiografia juu ya umbo la
dunia katika kazi yake maarufu ijulikanayo Surat
al-Ard. Kazi yake hii haijachapishwa ilikuwa kazi iliyoandikwa kwa mkono,
na ramani alizozichora bahati mbaya nazo
zilipotea lakini maelezo yake wanataaluma wengine waliweza kuunganisha na
kupata sura kamili ya ramani hizo alizozitaarisha.
Inafahamika kuwa aliwasimamia wasomi kama 70 katika somo la Jiografia katika kutekeleza
kazi hio ndio iliomwezesha kutengeneza ramani ya dunia ambayo ndio hii
inayotumika sasa, kazi zake zilipotafsiriwa kwa lugha ya Kilatino ndio ikatia
msukumo wa sayansi kusonga mbele katika nchi za magharibi.
Al-Khawarizimi ameweza kusaidia katika kuifanikisha kazi ilioanzwa na wataalamu wengine kujua nyakati kwa kutumia chombo kinachoitwa Sundial, chombo hicho ambacho hutumika kujua wakati katika siku wakati jua linawaka. Al-Khawarizimi alikitengeneza chombo hichi kwa njia nyengine kinyume na watangulizi wake wa Kihindi na Hellenistic. Kazi hii ya Sundial imetumika katika kujua nyakati za sala na huko nyuma kilikuwa chombo hicho kinawekwa juu ya Misikiti. Al-Khawarizimi alisaidia katika kuifanikisha kuiandaa kalenda ya Kiyahudi katika kitabu alichokiandika kinachojulikana Istikhraj Tarikh al-Yahud
Baadhi ya kazi zake ni pamoja na kitabu alichokiandika kwa kiarabu na kutafsiriwa kwa lugha ya Kilatino katika karne ya 12 kitabu hicho ni Kitab al-Jam'a wal- Tafreeq bil Hisab al-Hindi, kitabu hichi lau ingekuwa hakijafanyiwa tafsiri kwa Kilatino kingepotea wala kisingezungumzwa kwani maandishi ya awali ya kiarabu yalipotea. Kitabu chake cha Algebra kijulikanacho kama Al-Maqala fi Hisab-al Jabr wa-al- Muqabilah hichi kimesaidia sana wasomi wa nyakati zake nacho kilitafsiriwa kwa Kilatino kikiwa kimetoa mchango mkubwa wa sayansi kwa nchi za Magharibi. Msomi huyu aliweza kutengeneza Jadweli ya nyota na mwenendo wake na kutafsiriwa kwa lugha mbalimbali za nchi za Magharibi na kufanyiwa tafsiri hata kwa Kichina, bila ya kusahau ju ya kazi ya Sun-dials alipoandika kitabu kijulinacho Kitab al-Rukhmat.
Ukitaka kumuelewa Al-Khawarizimi na kuwafanya wasomaji wamuelewe itabidi kwa uchache uandike kitabu kisichopunguwa kurasa 2,000 ndipo utapoweza kumuelezea akafahamika, juu ya hayo azma ya makala hizi ni kutoa mwanga na kueleza kwa mukhtasari Waislamu na michango yao katika maendeleo ya dunia yetu hii.
Makala itakayofwata itamuangalia Ibn Battuta.
No comments:
Post a Comment