TATIZO NI MADRASA AU
NI AJENDA YA KUUDHURU UISLAMU?
Sehemu ya Kwanza
na
Kombo Hassan
Asalaam Aleikum,
Kila
sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu Swala na Amani zimfikiye Mtume
Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) na jamaa zake.
|
USULI
WA TATIZO
Historia ya Elimu ya Madrasa
Tanzania inasibiana na Historia ya kuenea kwa Uislam katika Afrika Mashariki
kuanzia Pwani hadi bara.
|
Kustawi
kwa Elimu ya Madrasa Afrika Mashariki:
|
Mwaka
1332, Mwarabu aitwaye IBN BATUTA alipotembelea Kilwa alikuta mji umekaliwa na
waliokuwa wakitumia lugha ya
Kiswahili. Baadaye miji ya Tanga,
Dar-es-Salaam, Mombasa, Lamu, Malindi, na Mikindani vikawa vituo vya
kueneza uislam na elimu ya kiislam katika miji ya Tanzania, Kenya, Uganda,
Rwanda, Zaire, Msumbiji, Malawi na Burundi.
Wajerumani walipofika Tanganyika waliwakuta Waislam
wanafahamu kuandika, kusoma na walikuwa wameelimika katika hesabu.
Mmishionari Ludwig Krapt alipofika kwa Chifu Kimweri wa Usambara mwaka 1848 walikuta
yeye na wanae wote wanajua kusoma. Rejea:
(I.N. Kimambo, na A.J.A. Temu, "History of Tanganyika," EAPH, Nairobi, 1969 uk.
126).
Herufi walizokuwa wakitumia zilikuwa za Kiarabu.
Wajerumani kwa ajili hii basi waliwaajiri Waislamu kama walimu, wakalimani na
makarani serikalini. Elimu hii yote na utamaduni wa ustarabu wa hali ya
juu ulikuwa unatokana na Uislamu na shule za Madrasa. Hapo ndipo ilipoanza
mbinu ya kuvunja maendeleo haya yote.
Herufi za Kiarabu zikapigwa marufuku kutumika na badala
yake watu wakalazimishwa kujifunza herufi za Kirumi. Muislamu ambaye jana
alipoingia kulala alikuwa anaitwa ameelimika akaamka asubuhi yake mjinga, hana
elimu, hajui kusoma wala kuandika. Njama zote hizi dhidi yaUislam ilikuwa
sehemu ya makubaliano kama ilivyoandikwa katika kifungu IV cha Mkutano wa Berlin wa mwaka 1884. Kifungu hicho kilikuwa
kinasema kuwa Ukristo ni lazima ulindwe dhidi ya Uislam. (Rejea: H.B Hansen, “Mission,
Church and State in Colonial Setting: Uganda 1890-1925,” London 1984, uk. 26,
vile vile angalia Ali M. Kirunda, Uganda Muslims and their Problems,” The
Monitor June 4-June 8, 1993).
Na wamishonari
walifuata nyayo za Madrasa na walimu wa kwanza katika shule za
misheni walikuwa Waislam ambao hawakusoma katika shule za kanisa bali katika Madrasa. Rejea: (Abel Ishuwi, “Education
and Social Change,” (1980).
Mwaka
1882, Waziri Mkuu wa Uingereza, Bw. Gladstone, akiwa ameinua juu Qur’an, alisema kuwaambia wabunge wa
Uingereza (House of Commons):
“So long as the Egyptions
have got this book with them, we will never be able to enjoy quite of peace
in that land.” (Muhammed Qutb 1972: xi)
Tafsiri:
“Madhali Wamisri wanacho
kitabu hiki hatuwezi kamwe kufurahia utulivu au amani katika nchi ile.”
Katika miaka 1900, kauli kama hiyo ilitolewa na Waziri wa
Makoloni ya Uingereza huko Uturuki pale aliposema:
“Muda wa kuwa Waislamu wanayo
Qur’an, basi watakuwa kikwazo kwetu. Kwahiyo ni lazima tuiondowe kutoka
maishani mwao.”
Marekani
na nchi nyingine za Magharibi zimekuja na mbinu ya kistratejia kama wahisani
kwa njia ya kuwashajihisha Waislamu kujioganaizi kwa kuwa na mtaala mmoja wa dini, kuanzisha “NGO’s” za ujasiriamali ili kuweza kukabiliana na
makali wa umasikini uliowapiga Waislamu wengi n.k.
Marekani
kwa kupitia aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa zamani Bw. Collin
Powell, na Waziri wa Ulinzi Bw. Dolnad Rumfeld, wamesema kuwa umadhubuti wa
Waislamu unatokana na wao kusoma, kufundisha, kuiamini na kuifuta Qur’an.
Hivyo ufumbuzi wa kudumu ni kuwatoa Waislamu katika Uislamu wao kwa kuingilia
mafundisho ya Qur’an. Na njia nzuri ni kuanzia kwenye Madrasa zao. Kampeni
hiyo iwe ya dunia nzima. Hapa tutaangalia tu wanayoyafanya Tanzania na
mafanikio yao ukilinganisha na yetu sisi Waislamu.
Njia
ya kwanza waliona ni kutoa misaada kwenye madrasa ili iwe ni mwanya na
hatimaye kubadilisha mitaala ya madrasa. Huko Kenya wakaenda kwa pupa kwa
balozi wa Marekani kutoa rundo la misaada ya vitabu na pesa kwa madrasa.
Waislamu wakashituka na wakakataa. Makafiri hawakukata tamaa walijifunza kosa
lao. Hapa Tanzania, wakaamua kuwa kwanza kabisa waanze na utafiti
utakaowajulisha ukweli halisi juu ya madrasa. Nawakaona ili Marekani
wasionekane waziwazi. Wakawatumia watu wengine, yaani Shirika la Kijerumani
liitwalo Konrad Adeneur Stiftung. Mwezi Mei/Juni 2003 walifanya utafiti wao
walioita “Qur’an Madrasa Baseline Survey.”
Yaani
utafiti wenye lengo la kujua hali halisi ya madrasa kwa Mkoa wa Dar es
Salaam. Waligundua mengi, lakini kwa sasa tuseme tu kuwa baadhi ya waliyojua
ni kuwa karibu ya nusu ya walimu wa madrasa wanapata mshahara wa mdogo. Wengine
hawalipwi kabisa. Theluthi mbili ya madrasa zinamilikiwa na watu binafsi na
zipo vibarazani. Kwa ufupi ni kuwa Serikali ya Marekani kwa kupitia Shirika
lake Liitwalo USAID linasaidia madrasa huko Zanzibar. Hivyo Waislamu
tunasaidiwa kwa kupitia mifuko mikubwa minne:
ð Mfuko wa Rais Bush wa Elimu ya Waislamu
(President Bush’s Muslim Education
Initiative).
ð Mfuko wa Rais Bush wa Kupambana na
Ugaidi Afrika Mashariki (President Bush’s East African Counter-terrorism
Initiative).
ð Skolaship za Balozi kwa Wasichana (The
Ambassador’s Girls’ Scholarship Program).
ð Mfuko wa Elimu Afrika (African
education initiative).
Wanazitumia
pesa hizo kuwasomeshea Waalimu wa Kiislamu, kuandaa mitaala na vitabu, kuwalipa
mishahara waalimu, na viongozi wa jamii, na kusaidia pia kipesa watoto wa
masikini. Wameanzisha pia Kituo cha Vitabu vya rejea vya Madrasa Zanzibar
(The Zanzibar Madrasa Resource Centre). Misaada hiyo Marekani kwa kupitia
mradi wa MKEZA (Mradi wa Kuendeleza Elimu Zanzibar) imekwisha kujenga madrasa
16 (mpaka mwaka 2007) moja ya madrasa hizo aliyotembelea mke wa Bush, Laura,
Julai 2005. Kwa mujibu wa USAID wenyewe Marekani ni wafadhili wakubwa kwenye
nyanda ya elimu huko Zanzibar.
***
Kwa
upande wa Tanzania bara USAID kwa kushirikiana na BAKWATA wametoa kitabu cha
Mwongozo wa kufundishia waalimu wa Kiislamu. USAID pia imetoa mafunzo
kwa waalimu 54 wa madrasa ya
kuwafundisha watoto wa kiislamu namana ya kupambana na UKIMWI. Mwongozo huo
waVitabu 2,500 uligawanywa kwa waalimu wa madarasa Dares Salaam na Iringa.
(Taarifa hizi zote zimepatikana kutoka
katika tovati ya USAID/Tanzania). Rejea: Islamic Propagation Centre (2007).
Kwa mujibu wa Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya
Amali (SMZ) kuhusu makadirio ya mapato
na matumizi ya fedha ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa mwaka wa
fedha 2013/2014:
“Elimu ya Madrasa na Vyuo vya Kuran
52. Mheshimiwa Spika,
Idara hii inashughulikia jumla ya madrasa/vyuo vya Kur- ani 2,251.
Aidha zipo skuli za maandalizi za madrasa 84, Unguja na Pemba
zinazosimamiwa na kuhudumiwa kupitia Kituo cha Zanzibar Madrasa Resource
Centre (ZMRC), ambazo ufundishaji wake unafuata misingi ya dini ya kiislamu.
53. Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2013/2014, Wizara kwa kushirikiana na Shirika la UNICEF
inakusudia kutoa mafunzo kwa walimu wa madrasa/vyuo vya Kur-ani 350, Unguja
200 na Pemba 150. Pia itaendelea kufanya ziara mbali mbali za kikazi katika
madrasa na vyuo vya Kur-ani pamoja na kusaidia kutatua changamoto
zinazowakabili pamoja na kushajiisha kufanya ziara za pamoja za kubadilishana
uzoefu.” (Mwisho wa kunukuu).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“217...Wala hawatoacha kupigana nanyi mpaka wakutoeni katika Dini yenu kama wakiweza. Na yeyote katika nyinyi akiacha Dini yake akafa naye ni kafiri, basi hao ndio ambao a'mali zao zimeharibika duniani na Akhera. Na hao ndio watu wa Motoni; humo watadumu.” (Al Baqara 2:217) ![]()
“120. Mayahudi hawawi radhi nawe, wala
Wakristo, mpaka ufuate mila yao. Sema: Hakika uwongofu wa Mwenyezi Mungu ndio
uwongofu. Na kama ukifuata matamanio yao baada ya ujuzi ulio kwisha kujia,
hutapata mlinzi wala msaidizi kwa Mwenyezi Mungu.” ( Al
Baqara 2:120).
Kwa
mujibu maelezo hayo hapo juu hii ni “Strategic Plan” (Mpango Mkakati) wa vita
dhidi ya Uislamu na Waislamu ili kulizivuga na kuingilia/kuharibu mafundi
yake ili ziwe ni zenye kuzalisha Waislamu “Mazezeta”.
HALI ILIVYO SASA KUHUSIANA NA MADRASA NA VITUO VYA KULELEA
WATOTO WALIO KATIKA MAZINGIRA MAGUMU
Hivi sasa hapa nchini
kumeibuka kadhia ya serikali kuzifunga
baadhi ya madrasa na vituo vya kulelea watoto walio katika mazingira magumu
nk. Hatua hiyo imechukuliwa kwa kile kinachodaiwa kutofuatwa sheria, kanuni
na sera za nchi.
|

No comments:
Post a Comment