Wednesday, 12 August 2015

KUTOKA JF: WAISLAM NA UCHAGUZI MKUU 2015 1


Quote By RUCCI View Post
Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini limekanusha taarifa iliyotolewa na Rajab Katimba kwamba baraza hilo linamuunga mkono mgombea wa CHADEMA, Edward Lowassa.

Katibu Mkuu wa Baraza hilo Sheikh Ramadhani Sanze alisema, hawahusiki na tamko hilo na Katimba sio msemaji wala katibu wa Baraza hilo.
Wanamajlis,
Huwezi kuchangia vyema mjadala huu kuhusu Baraza Kuu la Jumuiya na 
Taasisi za Kiislamu bila ya kwanza kujiua hustoria yake.

Nimejitolea kutoa darsa kuhusu Baraza Kuu ili sote tunufaike na tujue nini
khasa kinapelekea kufikia leo kunakuwa na kauli kama hizi katika umma wa 
Kiislam.

Tafadhali ingia hapa usome historia ya Baraza Kuu:
Mohamed Said: The Founding of Baraza Kuu (The Supreme Council of Islamic Organisations and Institutions of Tanzania)

Kwa mukhtasari Baraza Kuu liliundwa mwaka 1991 ili kuunusuru Uislam kutoka
mikono ya BAKWATA ambayo Waislam wengi waliikataa toka siku ya kwanza
ilipoasisiwa na serikali mwaka wa 1968.

Anaetaka kuijua historia ya BAKWATA anaweza kuipata hapa:
Mohamed Said: BAKWATA SEHEMU YA KWANZA

No comments: