Uonevu na Udini Upo
Tanzania
Na Alhaj Aboud Jumbe


Maandamano Maalim Aboud Jumbe, Maalim Aboud Maalim na Abdulrahman Babu
HOJA zimekuwa zikijengwa kuwa nchi yetu imefanikiwa kujenga utaifa ambapo hakuna ubaguzi wa kidini au kikabila. Aidha, Mtanzania yeyote ukimuuliza atakuambia kuwa serikali yetu haina dini. Kwa mtazamo huo viongozi hawaongozi kwa utashi wa dini zao kuwahujumu wananchi wasio katika dini moja.
Wanasiasa wanapotoa
shutuma dhidi ya watu, wanaodai wana udini, taswira inayojengwa ni k uwa
Muislamu ndiye mdini, bali Mkristo hawezi kuwa mdini. Ndio maana japo serikali
yaweza kuwa imejaa Wakristo ikilinganishwa na Waislamu, haionekani kuwa ni
tatizo.
Aidha, ndio maana
uongozi wa juu wa CCM una Wakristo wengi, lakini hausikii CCM ikiambiwa ni
chama cha Wakristo au kina udini. Lakini inapotokea chama kingine, kuwa na
viongozi Waislamu basi hubatizwa kuwa chama cha kidini.
Si wananchi wote
wanayoyatazama mambo kwa mtizamo huu. Wako wanaotoa hoja kuwa ubaguzi wa kidini
umekuwa ukifanyika, lakini kwa ustadi mkubwa.
Alhaj Aboud Jumbe, Rais
mstaafu wa Zanzibar, ametoa hoja kuonyesha kuwa Waislamu hawatendewi haki na
kwamba Kanisa Katoliki limepewa fursa ya pekee nchini.
Sehemu katika kitabu
chake inasema:
MTIRIRIKO
wa matukio ya kisiasa unaashiria agenda ya siri ambayo inaelekezwa kutumikia
Kanisa Katoliki ambalo siku zote linakuwa na uhusiano wa karibu na serikali
(hii) yenye kujenga mtizamo wa Kikristo ya Jamhuri ya Muungano na huku Waislamu
wakihasirika.
USHAHIDI
uliopo unaonesha kuwa Waislamu wa Tanzania Bara wamekuwa na uonevu ulioendelea
na kukoseshwa haki zao za msingi pamoja na kuwa katiba ya mwaka 1977 ilikuwa na
vipengele vya kuhakikisha haki za binadamu na usawa kwa raia wote.
Ushahidi
wa ziada unaonesha Kanisa nchini Tanzania ndilo linatowa maelekezo ya kisiasa
na mfumo wa kisiasa umekuwa ukitumiwa kutoa upendeleo kwa Wakristo ambao tayari
wamo katika kudhibiti nafasi mbalimbali katika asasi za umma.
Kama
tukichukulia maendeleo ya hali ya kisiasa nchini hivi sasa kuhusiana na
Muungano nina hakika ya kuwa na shaka kuwa utaratibu mzima wa kuwabana Waislamu
wa Tanzania Bara unaendeshwa kwa mbinu za mchwa sambamba na ule wa kuikaba
Zanzibar ili kuilazimisha kuingia katika mpango wa muda mrefu wa kuiingiza
katika serikali moja ili kuhakikisha Waislamu kutoka pande zote mbili za Bahari
ya Hindi hapa Tanzania wanasujudu kwa Bwana mmoja.
Sura
hii inataftishi suala la dini na siasa katika Jamhuri ya Muungano. Mada hii
huenda ikawaudhi baadhi ya watu. Lakini siku zote ukweli hauwafurahishi wale
ambao hawapendi ujulikane kwa sababu zinazoeleweka ambazo ni za kuchukiza za
kibinafsi na zenye makusudio maovu.
Tangu
nusu ya pili ya mwaka 1993 mashambulizi mbalimbali yasiyo na msingi yamekuwa
yakielekezwa na kuongezewa nguvu dhidi ya Waislamu maalum, lakini pia kwa
Uislamu kwa jumla.
Mashambulizi
ya awali yaliyofanywa na mtu binafsi, vikundi vya watu, vyombo vya dola na
mwisho vyombo vya habari yalielekezwa kwa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa
kujiunga na Jumuiya ya Mkutano wa Kiislamu (OIC).
Hii
ilikuwa ni rasharasha tu ya mabomu kabla ya matusi hasa hayajafuatia baadae.
Katika muda huo huo lilipitikana jaribio lililoshindwa ambapo uvumi usio na
msingi ulienezwa kuwa serikali ya Jamhuri ya Muungano ilitaka kujiunga na
Jumuiya nyingine ya Kiislamu inayoitwa Islam in Africa Organization (IAO), hili
likitowa mwanga, mashambulizi haya yalipangwa kulenga shabaha gani. Na ilikuwa
wazi kuwa waliojikita katika majadiliano hayo hawakuelekeza mabishano yao nje
ya Uislamu na Waislamu.
Kwa
mfano, kuwepo kwa ubalozi wa Vatican nchini Tanzania hakukupata kuhojiwa pamoja
na kuwa serikali hii inadai kuwa si ya kidini. Kanisa, CCM na serikali vyote
vimekaa kimya huku vikijua kutendeka kwa hilo lakini vikizibwa mdomo.
Kana
kwamba hiyo haikutosha kuonesha kuwa kuna mlalio dhidi ya upande mmoja, kulifuatia
jaribio la kumng'oa Rais Mwinyi kupitia taratibu za Bunge, kudai kufukuzwa Rais
wa Zanzibar Dk. Salmin Amour na baadhi ya Mawaziri wake na kelele za kuwataka
mawaziri Waislamu katika Jamhuri ya Muugano wajiuzulu kwa kutaka kusilimisha
Tanzania, inaonesha malengo ya mashambulizi hayo.
Mkakati
ukaandaliwa ambao ulitakiwa kuonesha kuwepo "kwa hila za Kiislamu"
ili kujenga hoja ya kuwasaka Waislamu ambao walionekana kuwa kero
isiyostahimilika. Fursa ilipopatikana basi ikatumiwa haraka. Uchokozi mbalimbali
dhidi ya Waislamu ambao mwengine haukuripotiwa ukaanza kuzua hisia tofauti za
wakandamizaji na wakandamizwaji kufuatia na ukamataji mkubwa na kesi katika
mahakama ambazo baadhi yake zimekuwa zikiendelea kwa muda mrefu.
Matukio
haya yamedhihirika kwa Waislamu wengi kuwa kumekuwa na hatua za makusudi
kuchanganya siasa na dini katika mambo ya serikali.
Kinyume
na kampeni inayosambazwa, Waislamu sio chanzo ila wao ni waathiriwa wa mbinu za
makusudi za kujenga mfumo wa uhasama ambao unazinyonya dini zote mbili na siasa
ili kuwabana Waislamu na pia kupata uwezo wa kuwakandamiza.
Dhana
ya kutenganisha dini na siasa katika wakati huu ilianzishwa na baadhi ya nchi
za Magharibi ili kuanzisha taifa lisilo na dini ili kuepuka uingiliaji wa
Kanisa ambao wakati huo ulikuwa ni mkubwa.
Awali
kitendo kama hicho kilionekana kama ni cha upinzani juu ya mamlaka ya Papa
ambae alikuwa ameigawa dunia, upande wa magharibi ukiwa kwa Uhispania iliyokuwa
na nguvu na upande wa mashariki kwa Ureno ambayo pia ilikuwa na nguvu na kuyaacha
mataifa makubwa ya Ulaya yakiwa yanakosa pahala pa kushika katika zama hizo.
Utaifa
mpya katika bara la Ulaya ulipingana na Papa na kundi lake kwa kuanza kuvamia
maeneo yaliyokuwa chini ya Uhispania na Ureno. Sio tu walianza kujitangazia
mamlaka zao huru, lakini pia walianza kujikatia maeneo mapya nje na ndani ya
Ulaya.
Baada
ya kufanikiwa kuunda mataifa yao walianzisha pia Makanisa yao ambayo yalikuwa
na lengo moja la kukuza dini. Kidogo kidogo mataifa haya "yasiyokuwa na
dini" yalianza kupeleka baadhi ya madaraka kwa wafalme, malkia na wabunge.
Wakati
ambapo kuna mgawanyo unaoeleweka na ulio wazi baina ya mamlaka ya kiroho na
kiserikali kwa upande wa dola na Kanisa, taasisi mbili hizo hazijaweza kusita
kuingilia mambo ya kidini, kiuchumi na kisiasa katika nchi zinazoendelea na
kusababisha hali ya kutoelewana, kutoaminiana, kukosekana kwa utulivu na pia
kusababisha fujo wakati wa utekelezaji wa mipango yao ya kihaini.
Hili
hutokea zaidi pale kunapokuwa na idadi kubwa ya Waislamu na Wakristo wanapoishi
pamoja. Tunaushahidi wa kutosha na usiopingika juu ya jambo hili kwa Tanzania.
Upitizi
wa makini wa kitabu "Kanisa Katoliki na siasa Tanzania Bara
1953-1985" unatoa habari za ndani zisizo za kawaida juu ya kampeni dhidi
ya Uislamu.
Kwa
maneno mengine kitabu hicho kwa kiasi fulani ni kukiri kwa yeye mwenyewe
mwandishi juu ya shughuli za Kanisa la Katoliki za kisiasa Tanzania, Kanisa
ambalo haliwezi kutenganishwa na Vatican na ambalo ubalozi wake ni mmoja katika
balozi kongwe nchini Tanzania.
Kwa
sababu zisizoeleweka kitabu hiki kimeandikwa na kuchapishwa na waumini wa
Kanisa hilo. Yaliyomo ndani ya kitabu hicho hayajakanushwa wala kubishiwa na
serikali ya Muungano ya Tanganyika au CCM, huu ukiwa ni ushahidi kamili juu ya
ukweli wa kukiri juu ya neno hilo.
Kwa
sababu na malengo yoyote ya kutolewa kitabu hicho , na lazima ziwepo sababu za
msingi za kufanya hivyo, kitabu hiki ni ufunuo mzuri juu ya mbinu za chini kwa
chini za Kanisa katika medani ya kisiasa Tanzania.
Kitabu
kinaeleza ni Kanisa Katoliki lililojenga njia ambazo ziliwawezesha kuwa na
mahusiano ambayo kitabu hicho inaeleza yalikuwa ya karibu kabisa na TANU wakati
wa miaka ya kupigania uhuru. Kinaonesha ni vipi Kanisa lilitayarisha waumini
wake shupavu ambao walikuwa wameshika karibu nafasi zote muhimu katika serikali
mpya ya Kiafrika ya Tanganyika.
Kinaeleza
ni vipi serikali ya Jamhuri ya Muungano ilirithi mfumo huo, na kuupanua kuingia
katika mamlaka ya Muungano na pia katika mambo yahusuyo Tanganyika. Na hapa
tunaweza kupata mwanga juu ya maana na ulazimishaji wa kuwepo serikali mbili
badala ya tatu kwa njia zilizogubikwa kama ilivyobainishwa na mkataba wa
Muungano (mapatano ya Muungano) na katiba zote zilizopitishwa Tanzania.
Hapa
ndipo unapoona kuna neno katika kudai kusimamishwa mfumo wa serikali moja.
Nguvu hizo zikapenya zaidi kupelekea Muungano wa ASP na TANU ambapo CCM
iliendeleza kazi za TANU kuhusiana na ushirikiano wa karibu na Kanisa Katoliki.
Kwa
wale viongozi, wawe wa Kanisa, CCM au serikali ya Muungano ambao walikuwa
wakijipigia kelele kutenganisha kwa siasa na dini, lakini wao wenyewe wakiwa
ndio waendelezaji wakubwa wa hilo, wana kazi ngumu ya kuelezea kwa umma kwa
ujumla lakini zaidi kwa Waislamu. Sivalon anaelezea juu ya mpango na njama zinazoendelea
zikishirikisha Kanisa Katoliki, Chama (TANU-CCM) na serikali ya Muungano.
Tangu
njama hizo ziwekwe wazi 1992 hapakuwa na kauli moja ya kupinga au kutolea
maelezo juu ya hilo. Huku ni kukiri kwa dhahiri juu ya mipango na njama za
Kanisa zinazofanywa hali zikiwa zinaeleweka na mkono wa chama na serikali yake.
Yafuatayo
ni baadhi ya madondoo kutoka kitabu hicho:
"Mwishowe
tutakuja kuonesha jinsi Rais mstaafu Nyerere alivyokuja kuwa kiungo cha pekee
kati ya chama/kanisa na Kanisa Katoliki. Uhusiano huo unaelezwa kwanza kama
msingi wa kuelewa jinsi gani na kwa kiasi gani viongozi wa Kanisa
walivyoingilia kati maendeleo ya siasa hapa Tanzania (uk. 5).
Huo
uhusiano ukawaweka viongozi wa Kanisa katika nafasi nzuri ya kuelekeza
maelekezo ya siasa Tanzania. (uk. 9).
Aboud Jumbe na Mwandishi 2000 |
No comments:
Post a Comment