Haiwezekani
kuielewa ahadi ya Nyerere katika haki na usawa kwa raia wote kama alivyoahidi
wakati wa kudai uhuru, hadi usome hotuba yake aliyoitoa tarehe 10 Desemba, 1962
katika Bunge wakati Tanganyika inakua jamuhuri. Hotuba ya Nyerere ilijikita
kwenye matatizo ya upogo kati ya Waislam na Wakristo. Nyerere alifanya hivi
labda akijua kuwa ingawa yeye alikuwa Rais Mkatoliki lakini waliomuweka
madarakani kuitawala Tanganyika walikuwa Waislam. Nyerere alikuwa na haya ya
kusema:
Hakuna
njia nyepesi ya kuondoa tafauti baina ya raia wetu Waafrika na wasio Waafrika;
hakuna njia nyepesi ya kuondoa tofauti za elimu kati ya Wakristo na Waislam, au
baina ya wachache wenye elimu na wengi wa watu wetu wasio kuwa na elimu; hakuna
njia nyepesi ambayo Wamasai na Wagogo wanaweza wakalingana na Wahaya na
Wachagga na Wanyakyusa.
Hii
ilikuwa kauli ya serikali ya kudhihirisha nia yake njema. Kauli hii ilikuwa ya
kuwapa matumaini na kuwahakikishia Waislam na wale wote walioathirika na dhulma
ya wakoloni, kuwa serikali ilikuwa inatambua shida zao na itachukua hatua
zifaazo kurekebisha hali hiyo. Wakati Nyerere anatoa kauli hii ya kutia moyo, serikali
iliyokuwa imejaa viongozi wa Kikristo na taasisi za Kikristo zilikuwa imejaa
hofu wakiogopa harakati za Waislam za kujiletea maendeleo zilizokuwa
zinatapakaa nchi nzima kwa kasi. Walifahamu fika nguvu na umoja wa Waislam
ukitumiwa vyema hapana shaka Waislam watakuja juu. Kwa viongozi wa Kikristo
waliokuwa wameshika madaraka ya serikali hii ilimaananisha kugawana madaraka
sawa na Waislam, kwao wao harakati hizi mpya ziliashiria kuanguka kwa himaya
yao katika madaraka kama viongozi.
(Kutoka:
Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes (1924 – 1968)…)
No comments:
Post a Comment