Sunday, 19 June 2016

WATOTO WA WAPIGANIA UHURU BI. MAUNDA PLANTAN, JUMA MWAPACHU, HAPPY MTAMILA NA KLEIST SYKES WANAPOWAKUMBUKA WAZEE WAO


Juma Mwapachu na Julius Nyerere













Nguruvi3,
Ama ingekuwa si kwa kuwa naburudika kufanya mjadala na wewe
mie muda mrefu ningelikwisha nyanyua mikono juu lakini nastarehe
kuongea na wewe.

Allah amekupa kipaji cha aina yake.

Majibu nimekupa kuhusu katiba ya TAA Political Subcommittee kuwa
nyaraka na microfilm zote hazionekani Maktaba ya CCM Ddodoma
na TNA.

Sikuishia hapo nimekueleza kuwa kabla yangu katiba hiyo ilitajwa na
Listowel mwaka wa 1965 na Pratt 1976.

Bado unataka nikuletee hiyo document.
Kama wewe hodari sana mbona huwaulizi CCM nyaraka hizo zilipo?

Lakini ninastarehe katika mnakasha huu kwa kuwa natoa darsa na
wengi wanasoma historia ambapo hawakupatapo kuisikia hata kwa
mbali.

Ndiyo maana narudi hapa tena na tena na tena.
Nakushukuru sana kwa hili.

Sasa nisikilize kwa makini na tuliza ubongo wako nikufunze mbinu
za ''critical analysis'' na kujifunza kusoma katikati ya mistari.

Sitakujibu hayo yote uliyoandika nitakujibu hayo tu ambayo umeweka
rangi nyekundu.

Hamza Mwapachu alimjulisha Nyerere kwa uongozi wa TAA 1949.

Akili yako mara moja imekwenda kuwa walikuja hadi New Street na
kuzungumza na Mwalimu Thomas Saudtz Plantan aliyekuwa rais na
Clement Mohamed Mtamila aliyekuwa katiibu wa TAA wakati ule.

Lakini ukweli ni kuwa Mwalimu Thomas Plantan na Clement Mtamila 
walikuwa hawajapata kukutana na Nyerere hadi alipokuja kwa Abdul
Sykes 
1952.

Inawezekana ujulisho huo ulikuwa wa salam za mdomo au wa barua.

Nakuwekea picha nikifanya mahojiano na Bi. Maunda Thoams Plantan
mtangazaji wa kwanza wa kike Tanganyika, Sauti ya Dar es Salaam 1952
na mwalimu wa shule.

Mjukuu wa Affande Plantan na mtoto wa Mwalimu Thomas Saudtz
Plantan
.

[​IMG]
Kushoto Bi. Maunda Plantan na Mwandishi

Katika mazungumzo yetu hakupatapo kunambia kuwa baba yake
alipata hata kwa siku moja kuonana na Nyerere.

Nimezungumza pia na Happy Mtamila hata mara moja hajanieleza
kama baba yake alipata kuonana na Nyerere kabla ya 1952.

[​IMG]
Kulia Bi. Happy Mtamila na Mwandishi

Ningependa kukufahamisha tu kuwa uamuzi wa Nyerere kuacha kazi
ulifanyika nyumbani kwa Clement Mtamila Mtaa wa Kipata na Sikukuu.

Nyumba hii ilikuja kununuliwa na ukoo wa Baharoon ikavunjwa na
sasa ni ghorofa. 

Kushoto: Kleist Abdulwahid Sykes, Ebby Abdulwahid Sykes, Saudtz
Thomas Plantan na Abdulwahid Ally Sykes

No comments: