Hewalaa, ni kweli ni Juma Mwapachu aliyekuletea habari hiyo. Nimefanya editing ya hoja zangu kwa kuondoa jina Bakari na kuweka Juma, Mwapachu ikibaki pale pale,hoja ni hizi hapa chini
Wanajamvi
Mnakasha umefikia mahali patamu sana.
1. Tunasubiri Mohamed Said atuletee nakala ya draft(rasimu) au katiba ya kuandika au kukopi iliyokuwepo, andikwa au tumiwa na Abdul Sykes kabla ya katiba iliyoandikwa/kopiwa na Nyerere.
2. Tunasubiri Mohamed Said atueleze kabla ya kutangazwa kwa TANU mwaka 1954, jina la TANU lilitumika katika mkutano au mkusanyiko gani ambao Adul Sykes au mwingine nje ya Nyerere
3. Halafu kuna sauti hii ya Mohamed Said katika dakika 51-53 akimueleza mtangazaji wa radio kuwa kabla ya mwaka 1952 hakuna aliyemsikia au kumjua Nyerere. Sikiliza hapa
https://soundcloud.com/mwinyimadi/sheikh-hassan-bin-amir-nur-fm
Kisha usome maneno haya ya Juma Mwapachu aliyempa Mohamed Said atueletee kama zawadi. Lengo lilikuwa kuonyesha sisi 'vichekesho' hatujui na wala hatuna mawasiliano na watu wakubwa kama akina Mwapachu.
Hata hivyo, katika maandishi hayo tunapata habari nyingine ikihusiana na introduction iliyofanywa na Hamza Mwapachu kwa Nyerere katika kile alichosema TAA Leadership
Kumbuka TAA leadership wakati huo ilikuwa chini ya Abdul Sykes, hivyo Hamza Mwapachu alimjulisha Nyerere kwa Abdul Sykes kama sehemu ya TAA leadership.
Soma hapa maneno ya Juma Mwapachu
''I still recall the visit vividly. I was a standard three pupil then and together with my brother Bakari had to sleep in the sitting room leaving our bedroom to the two guests.
Abdul Sykes was then President of TAA and the TAA leadership plus Dar-based political activists who were predominantly Moslems wanted Abdul Sykes to retain the Presidency.
Abdul was eager to secure Hamza's position on
the matter given the fact that it was Hamza who introduced Nyerere to the TAA leadership in Dar back in 1949 before Nyerere left for Edinburgh University''
Kwa faida ya wasomaji, tunaweka maneno ya Juma Mwapachu katika tafsiri isiyo rasmi
Tunaomba radhi ikiwa kuna mapungufu yatakayojitokeza. Juma Mwapachu anasema hivi
''Bado nakumbuka kwa uyakinifu. Nilikuwa mwanafunzi wa darasa la tatu na pamoja na kaka yangu Bakari tulilala sebuleni kuacha chumba kwa wageni wawili.
Abdulwahidi alikuwa Rais wa TAA na uongozi wa TAA pamoja na wanaharakati wa siasa wengi wao wakiwa waislam walitaka Abdul Sykes abaki kuwa Rais
Abdulwahid alikuwa tayari kumuafiki Hamza katika suala hilo katika ukweli kuwa ni Hamza ndiye aliyemtambulisha Nyerere kwa uongozi wa TAA Dar es salaam mwaka 1949 kabla Nyerere hajaondoka kwenda chuo kikuu Edimburgh''
Ndipo tunakuja kutafuta ufafanuzi kwa Mohamed Said katika hoja ya 4 na 5
4. Mohamed Said , je bado unaamini kuwa kabla ya 1952 hakuna yoyote aliyewahi kumsikia Nyerere katika TAA HQ chini ya Abdulwahid Sykes?
5. Je, maneno ya Juma Mwapachu ni uzushi au ni ukweli?
6. Ikidhihirika J.Mwapachu maneno yake ni sahihi,utaliomba radhi jamvi kwa upotoshaji?
Je, utawaomba radhi wasikilizaji uliowapotosha katika redio na lini utafanya hivyo?
7. Kama maneno yako ni nkweli, je utakuwa tayari kukanusha maneno ya Juma Mwapachu hapa jamvini na kutuomba radhi kwa kutuletea habari zisizo na ukweli?
Na mwisho, Mohamed ajibu hoja hizi, hatuwezi kuburuzwa tu tukubali hata upotoshaji eti kwavile tunataka kujua mengine.
Haina maana kujua mengine ikiwa yapo tusiyoyajua kama haya tunayomuuliza
Mohamed Said, tafadhali sana usihamishe mjadala na kukwepa hoja.
Tunataka kusahihisha historia ya kivukoni kwa ukamilifu wake.
Hatutaki kuwaacha vijana wamechanganyikiwa kwa hoja kinzani.
Tutaendelea baada ya majibu, vinginevyo ukiri makosa kama tunavyokubali ya kivukoni.
Ahsante
.
No comments:
Post a Comment