Sunday 26 March 2017

KUTOKA WHATSAPP GROUP: EMPIRE CINEMA SHULE BAADA YA DARASA LA SHULE


Sheikh Mtoro tupoe sote kwa kuondokewa. Binafsi miezi mitatu hii nimeondokewa na watu wangu wa karibu watatu ambao tumekuwa na kucheza pamoja, wawili - Eyshe Abbas Max na Mohamed Awadh Chico, Mohammed Ali Muhsin huyu tumejuana tuko vijana. 
Elvis Presley. ..

Kaka kwa wale wa miaka ile wanajua Eid ilikuwaje Dar es Salaam kuanzia Mnazi Mmoja kwa ''Karagosi Kalewa Tembo,'' hadi kwenye ''theatres'' mjini. Chips pale sasa Mbowe nk nk.
Nilikuwa na miaka 12 mwaka wa 1964.

NIkaingia Empire kumuona Elvis katika ‘’Blue Hawaii.

Kuanzia siku ile hatukuachana hadi alipofariki 1977.

Nikiimba nyimbo zake nyingi. Nakumbuka siku ya pili nakunywa chai na marehemu baba yangu siku hizo tukikaa Lindi Street mkabala nyumba yetu na International Hotel inakaribia Nkrumah Street.

Mtaa huu ndipo marejemu Ally Sykes alikujwa na ofisi yake na Peter Colmore High Fidelity (Makao Makuu yakiwa Government Road Nairobi) na ndipo nilipomjua Peter Colmore kwa karibu.

Basi nampa mzee stori za Elvis na ‘’Blue Hawaii.’’ Yeye ananisikiliza tu.

Mwisho akanambia kuwa wao enzi zao mjanja wao alikuwa Bing Crosby.

2011 nimekaribishwa kusomesha darasa la ‘’Undergraduates,’’ University of Iowa Marekani  mwenyeji wangu ni Prof. James Giblin alinambia kabla, Waamerika hupenda kumjua mtu ''backgroud'' yake kabla hawajaingiliananae.

Mkewe na yeye ni ''lecturer,'' pia akanambia hilo darasa hao wanafunzi ni watoto wa ''millionaires'' nisishangae nikiwoana hawana adabu.

Ananambia wazee wao wametutupia sie walimu ulezi wa watoto wao maana karibu wote ni watoto vigego yaani hawasikii.

Basi nimetayarisha ''slide.''

Slide ya kwanza kwenye ''screen,'' ‘’poster,’’ ya Blue Hawaii wanashangaa vipi huyu Mwafrika na Elvis wapi na wapi?

Nawaambia, ''It was Elvis and this movie which made me pick up the guitar.''

Mshangao unaendelea na ''curiosity.'' Picha ya pili mimi mwenyewe ''on stage with ''The Rifters...1969...

'' Sir that's you with tha band?''

Sote sasa tuko ''relaxed,'' wanafunzi wanaona ala huyu kumbe ''crazy,'' mwenzetu...''

Lecture ikaanza, ''Islam and Politics in Tanzania The Struggle for Independence.''
Empire kaka movie nyingi tumeona pale hasa ''Westerns,'' enzi za Gemma, Django nk. nk.

Rafiki yangu Abdallah Mkwanda (Ingemar Johansson) alikuwa heshi kunikumbusha ''All The Young Men'' aliocheza Allan Lade movie aliyoiona Empire Theatre.

Siku zimepita.

No comments: