Mswada wake huu ulichukua miaka
24 hadi 1973 kufikia kuchapwa na kama si juhudi za John Iliffe mswada ungebaki
kama ulivyoandikwa na mwishowe kutoweka kama zilivyotoweka nyaraka nyingi
katika historia ya Waafrika wa Tanganyika. Mswada huu ulichapwa katika kitabu
alichohariri Iliffe, ‘’Modern Tanzanians,’’ Kilichopigwa chapa na Tanzania
Publishing House. Nyaraka hizi za Sykes zimesaidia sana katika kuhifadhi si
historia hii ya African Association bali hata historia ya TANU. Abdul Sykes
alimpa mswada huu pamoja na nyaraka nyingine binti yake Daisy, wakati ule
mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na kupitia nyaraka hizi mwalimu wake wa
historia, John Ilife aliweza kujua mengi ambayo yalimsaidia katika kuiandika
kwa uhakika historia ya African Association. Nyaraka hizi ndizo nyaraka pekee
zilizoweza kuhifadhiwa kutoka kwa waasisi wa African Association waliokuwapo
kati ya mwaka wa 1929 hadi 1954 ilipokuja kuasisiwa TANU.
Erika Fiah
Mswada wake huu ulichukua miaka
24 hadi 1973 kufikia kuchapwa na kama si juhudi za John Iliffe mswada ungebaki
kama ulivyoandikwa na mwishowe kutoweka kama zilivyotoweka nyaraka nyingi
katika historia ya Waafrika wa Tanganyika. Mswada huu ulichapwa katika kitabu
alichohariri Iliffe, ‘’Modern Tanzanians,’’ Kilichopigwa chapa na Tanzania
Publishing House. Nyaraka hizi za Sykes zimesaidia sana katika kuhifadhi si
historia hii ya African Association bali hata historia ya TANU. Abdul Sykes
alimpa mswada huu pamoja na nyaraka nyingine binti yake Daisy, wakati ule
mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na kupitia nyaraka hizi mwalimu wake wa
historia, John Ilife aliweza kujua mengi ambayo yalimsaidia katika kuiandika
kwa uhakika historia ya African Association. Nyaraka hizi ndizo nyaraka pekee
zilizoweza kuhifadhiwa kutoka kwa waasisi wa African Association waliokuwapo
kati ya mwaka wa 1929 hadi 1954 ilipokuja kuasisiwa TANU.
African Association kabla ya
Vita Kuu ya Pili (1914 – 1938) ilipitia misukukosuko mingi ya uongozi. Viongozi
wenyewe kwa wenyewe walikuwa wanagombana kwa kupishana mitazamo na migongano ya
haiba. Maarufu katika migongano hii ni ugomvi wa mwaka wa 1933 kati ya Kleist
na Erika Fiah ikapelekea Kleist kususa chama kabisa hadi alipoandikiwa barua na
Mzee bin Sudi aliyoainza kwa ‘’Bismillah RahamanRahim, ‘’ akimuomba Kleist
arejee kwenye chama. Mzee bin Sudi wakati ule alikuwa ndiyo rais wa African
Asociation. Erika Fiah alikuwa Mganda
aliyeingia Tanganyika na majeshi ya Uingereza katika Vita Vya Kwanza. Huyu Fiah
alikuwa na fahamu nzuri sana na inaaminika ni katika ‘’ma-leftist,’’ wa mwanzo,
watu walioingiza siasa za kikomunisti Tanganyika. Erika Fiah alikuwa na gazeti
lake mwenyewe, ‘’Kwetu,’’ na yeye binafsi akiwa mhariri.
Gazeti hili lilikuwa mfupa wa
kooni kwa serikali ya Kiingereza. Fiah alikuwa bingwa wa vijembe na wakati
mwingine hata kwa Waafrika wenzake na aliyepata kipigo hiki sana alikuwa
Kleist. Yawezekana kwa ajili ya biashara alizokuwanazo Kleist na kutokana na
msimamo mkali wa Fiah kama mtu wa mrengo wa kushoto, Fiah alihisi Kleist
hakufaa kuongoza African Association kwa ule ‘’ubepari wake.’’ Vijembe vya Fiah
katika gezeti lake vikawa havipungui ndani ya kurasa za Kwetu. Fiah katika
hamasa zake alipata kujaribu hata kuwaunganisha wakulima na wafanyakazi wa
Tanganyika dhidi ya Waingereza. Juu ya hali hii ya siasa mjini Dar es Salaam lakini
mahafali hawa wawili wote kwa macho ya wenyewe wenyeji wenye mji wao wa Dar es
Salaam kama Wazaramo, Wamashomvi, Wandengereko na Warufiji hawa walikuwa, ‘’watu
wa kuja,’’ wakiwaona hodari wa kujitiatia katika mambo kutaka wao siku zote
wawe viongozi. Ukiangalia utaona jinsi ukoloni ulivyokuwa na uhodari wa
kuwagawa watu ili watawaliwe kirahisi.
Thomas Saudtz Plantan
Ndani ya uongozi wa African
Association kulikuwa na watoto wa askari wa Kizulu waliokuja na Herman Von
Wissman kutoka Mozambique na Sudan mwishoni mwa miaka ya 1800. Hawa walikuwa akina
Kleist Sykes, watoto wa Plantan kama Thomas, Schneider na Mashado; na Hassan Machakaomo. Kulikuwa na Wanubi kama Ibrahim
Hamisi na Wamanyema kama Mzee bin Sudi. Fiah hulka yake hii ya kuwashambulia
wenzake ili furtu ada pale alipomshambulia Martin Kayamba alipokufa katika
taazia aliyoaindika na kumweleza Kayamba kama kibaraka wa Waingereza ambae
wananchi wa Tanganyika hawakunufaika no lolote kutola kwake si kwa elimu yake
wala madaraka makubwa aliyopewa na Waingereza. Fiah alikuwa kiboko.
Hawa watoto wa Kizulu na Kinubi
walisomeshwa katika shule za Kijerumani na wakawa wanasema Kijerumani kama
maji. Hii iliwanyanyua na wakawa katika ule ukoloni wao wana nafasi nzuri
katika jamii ya kuweza kuwa na kazi za maana ukilinganisha na mathalan,
Wamashomvi waliokuwa maarufu kwa biashara ya soko ,(kiasi kuwepo kwa msemo
kuwa, ‘’Mmashomvi mmoja hawezi kufunga soko,’’)na Wandengereko. Hapa tayari
tabaka lilikuwa lishajengeka. Palikuwa na magomvi mengi baina ya hawa watu, ‘’wakuja,’’
na ‘’wenye mji,’’ kufikia hadi kugombana katika Al Jamiatul Islamiyya fi
Tanganyika ambao ulikuwa umoja wa Waislam wa Tanganyika chama ambacho Kleist
alikiasisi mwaka wa 1933 akiwa katibu muasisi na Mzee bin Sudi akiwa rais. Hali
hii ya sintofahamu iliwafurahisha mno Waingereza kwani vita vya panzi furaha
kwa kunguru. Sasa ikiwa siasa zilikuwa hivi vipi watu hawa watajiunga kuunda cha kimoja
cha siasa chenye nguvu kupambana na ukoloni? Waswahili wana msemo, ‘’Mungu si
Athumani.’’ Waingereza watajikwaa na huku kujikwaa kwao ndiko kutawaleta Waafrika
wa nchi nzima kuwa kitu kimoja. In Shaa Allah tutafika huko baadae.
Kulia: Abdul Sykes na mdogo wake Ally wakiwa Burma
Vita Kuu ya Dunia
Lakini huu ushawishi wa Wazulu
na Wamanyema katika African Association haukumalizika haraka hata kidogo ingawa
kufikia baada ya Vita Kuu ya Pili wakati sasa wasomi wa Makerere walipoanza
kujiingiza katika siasa katika TAA misuguano hii ya ‘’uzawa,’’ pole pole na kwa
taratibu ikaanza kupotea kwani upepo mpya ulikuwa unavuma Afrika. Waafrika
walianza kuwaza kudai nchi yao na vijana wa Makerere walitegemewa kwingi kama
wangeliongoza vita hivi. Lakini Makao Makuu ya TAA New Street palikuwa bado na
uongozi wa wazee wa enzi ya Wajerumani na uongozi huu ulikuwa umechoka. Rais
alikuwa Mwalimu Thomas Plantan na Katibu wake alikuwa Clement Mtamila. Uongozi
huu haukupigwa vita na watu kutoka mbali la hasha. Schneider Abdillah Plantan
mdogo wake Mwalimu Thomas Plantan alisimama kidete kuona kuwa TAA inashikwa na
vijana. Uongozi huu uliangushwa na Dr. Vedasto Kyaruzi akachaguliwa katika
Ukumbi wa Arnautoglo rais wa TAA na Abdul Sykes Katibu. Kaondoka Mzulu, Mwalimu
Thomas Plantan katika uongozi ambae alikuwa ni baba yake Abdul katika ukoo akaingia
Abdul mtoto wa Kleist ambae yeye ni Mwalimu Thomas Plantan ni ndugu yake na kuna
wakati kwa kuwa Kleist alilelewa na Affande Plantan toka mtoto machanga baada
ya baba yake kufa njiani wakati wakitoka katika kupigana na Chief Mkwawa
Kalenga, Kleist akijulikana kama Kleist Plantan. Kigingi cha kuweka msingi wa
kuunda TANU ulisimikwa kipindi hiki mwaka wa 1950 kwa fikra aliyokujanayo Abdul
kutoka Burma akiwa askari wa King’s African Rifles (KAR).
Earle Seaton na Mwalimu Julius Nyerere
Mwaka huu wa 1950 utaingia
katika historia kuwa ndiyo mwaka ambao viongozi wa TAA waliikabili serikali ya
kikoloni na mapendekezo ya kutaka wakabidhiwe nchi yao kama sheria za nchi
zilizokuwa chini ya Udhamini wa Umoja wa Mataifa zinavyoelekeza. Tanganyika
ilikuwa Mandate Territory chini ya uangalizi wa Uingereza na wakati wakiwa
tayari kujitawala Waingereza sharia iliwalazima kuipa Tanganyika uhuru wake.
Hiki ni kisa kirefu kukieleza lakini muhimu ni kueleza kuwa uongozi wa Dr.
Kyaruzi na Abdul Sykes uliunda ndani ya TAA Political Subcommittee ambayo
ilipeleka kwa Gavana Edward Francis Twining mapendekezo ya katiba yaliyoshauri Tanganyika
ipewe uhuru wake baada ya miaka 13 huku kukiwa na uchaguzi wa kura moja mtu
mmoja katika kuchagua wajumbe wa LEGCO.
Wajumbe wa Kamati Ndogo ya Siasa katika
TAA walikuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Amir, Abdul Sykes, Hamza
Kibwana Mwapachu, Sheikh Said Chaurembo, Dr. Vedasto Kyaruzi, Stephen Mhando na
John Rupia. Katika kamati hii alikuwapo mjumbe mmoja ambae hakuwa akitokeza
lakini yeye ndiye alikuwa mshauri mkuu katika mambo yote ya sheria na katiba
kuhusiana na Nchi Chini ya Udhamini wa Umoja wa Mataifa. Mtu huyu jina lake
lilikuwa Earle Seaton.
Kushoto Mwandishi akiwa na Dome Okochi Ruiru, Nairobi 1972
Mwaka wa 1952 Wazungu Meru
waliwadhulumu Wameru ardhi yao na Wameru walikataa kudhulumiwa. Kaimu Rais na
Katibu wa TAA Abdul Sykes alimuomba Earle Seaton atoe msaada kwa Meru Citizens’
Union chama kilichokuwa kinaongozwa na Japhet Kirilo kupinga dhula ile na
Seaton akiongozana na Japhet Kirilo walifikisha malalamiko yao UNO na Kirilo
alizungumza mbele ya Kamati ya Udhamini, Seaton akiwa mkalimani wake. Wameru
hawakupewa haki yao na hapa ndipo walipojikwaa Waingereza. Abdul Sykes aliunda
kamati iliyomjumuisha mdogo wake Abbas Sykes, Saadan Abdu Kandoro na Japhet
Kirilo iliyotembea nchi nzima kueleza dhulma ile na madhila mengine ya ukoloni.
Suala la ardhi ya Wameru liliwasha moto nchi nzima. Fikra ya kuunda chama cha
siasa aliyokuwanayo Abdul Sykes, Ally Sykes, Hamza Mwapachu na wazalendo
wengine pale Makao Makuu ya TAA New Street ikawa sasa imepata mahali pa
kushika. Yako mengi katika historia hii ya kuundwa kwa TANU lakini si rahisi
kueleza yote hapa. Inatosha kueleza kuwa Nyerere alipofika nyumbani kwa Abdul
Sykes mwaka wa 1952 akiwa na barua ya utambulisho kutoka kwa Hamza Mwapachu
hali ya siasa Tanganyika ilikuwa kama moto wa makumbi ukiwaka chini kwa chini.
Mwaka wa 1953 ulifanyika
Uchaguzi wa kuwania urais wa TAA. Julius Nyerere alikuwa anagombea nafasi ile
dhidi ya Abdul Sykes aliyekuwa kaimu rais baada ya Kyaruzi kuhamishwa Dar es
Salaaam ili kupunguza nguvu ya TAA. Uchaguzi huu ulikuwa tarehe 17 April kwenye
Ukumbi wa Arnautoglo. Nyerere alishinda kwa kura chache sana. Hiki ni kisa cha
kusisimua sana lakini hapa nafasi haitoshi kukieleza. Ila inatosha kusema kuwa
safari ya kuelekea Saba Saba 1954 kuunda TANU ilikuwa imewiva. Mwaka ule wa
1953 viongozi wa TAA walikuwa hawa wafuatao: J. K. Nyerere, Rais, Abdulwahid
Sykes, Makamu wa Rais; J. P. Kasella Bantu, Katibu Mkuu; Alexander M. Tobias na
Waziri Dossa Aziz, Katibu wa pamoja wa muhtasari; Wajumbe wa kamati: Dr Michael
Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said Tewa, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C.
Ongalo na Patrick Aoko.
Mwaka wa 1954 tarehe 7 Julai,
1954, TAA ilikutana Makao Makuu New Street kujadili katiba mpya ya chama kipya
cha siasa - TANU. Jimbo la Mashariki ambalo liliwakilishwa na, ndugu wawili
Abulwahid na Ally Sykes, Dossa Aziz, Tewa Said Tewa, Patrick Kunambi, Kasella
Bantu, John Rupia, Julius Nyerere na C. O. Milinga; Jimbo la Kaskazini
liliwakilishwa na na Joseph Kimalando na Japhet Kirilo; Jimbo la Ziwa
liliwakilishwa na Abubakar Kilanga, L. M. Makaranga. Katika wanachama 17
waasisi, 9 kati yao walitoka Makao Makuu, 5 walitoka Jimbo la Ziwa, 1 alitoka
Jimbo la Magharibi na 2 Jimbo la Kaskazini. Huu ukawa ndiyo mwisho wa safari
iliyoanza mwaka wa 1924 na Dr. Aggrey alipomshauri Kleist Sykes kuunda Umoja wa
Waafrika wa Tanganyika ambao Kleist aliuunda African Association mwaka wa 1929
akishirikiana na wenzake wengi wao wakiwa marafiki zake.
Waasisi wa TANU 7 Julai, 1954
Kulia Daisy Abdulwahid Sykes na Mwandishi Daisy akiwa ameshika kitabu cha maisha ya baba yake
Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) alichoandika Mwandishi
No comments:
Post a Comment