Saturday 14 October 2017

BI. FATIMA MATOLA MAMA MPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA ASIYEJULIKANA

Hapo chini ni nyumba ya Bi. Fatima Matola mwanachama wa TANU  mazalendo aliyepigania uhuru wa Tanganyika.

Baba wa Taifa alikuwa akifikia nyumba hii wakati wa kupigania uhuru.
Nani keshapata kusikia jina hili la Bi. Fatima Matola?

Kuna hotuba ya Baba wa Taifa anasema kuwa safari yake ya kwanza baada ya kuundwa TANU mwaka wa 1954 alikwenda Mbeya.

Lakini Nyaraka za Sykes zinaonyesha kuwa safari ya kwanza ya Baba wa Taifa ilikuwa Mororgoro akifuatana na Zuberi Mtemvu.

Kuna barua ya tarehe 15 Agosti, 1954 mwezi mmoja tu baada ya kuundwa TANU kutoka kwa  Mtemvu akimwandikia Ally Sykes, Mtemvu akieleza matatizo waliyoyapata yeye na Nyerere Morogoro katika kuitangaza TANU. 

Hii ndiyo safari ya kwanza ya Baba wa Taifa katika kuitangaza TANU na safari ya pili ilikuwa Lindi.

Ikiwa safari hii ya Mbeya kwa namna yoyote ilikuwa ndiyo ya kwanza basi Baba wa Taifa alifikia nyumbani kwa Bi. Fatima Matola ambae nyumba yake ndiyo hiyo hapo chini kwenye picha. 

Kuna mtu yeyote anaemfahamu shujaa huyu wa ukombozi atupe historia yake?


Picha kwa hisani ya gazeti la Tanzania Daima Jumamosi Oktoba 14, 2017

No comments: