Sheikh Ahmed Islam |
Ushuhuda wa kweli👇
Innaa
lillaah wainnaa ilayhi raajiuun
Abul
Fatma... huo ni msiba mkubwa sana, kwa kweli tumefiwa na mzee mchamungu.
Mimi
Kalezi Hemedi, nilipata bahati ya kumjua, na ninadiriki kusema alichokisema Dr
Dau ni ukweli mtupu.
Hapa
nina uchungu mkubwa sana, Mzee Islam katutoka...?
Alhamdulillah... ninawajibika kesho kwenda Dar inshaallah.
Nitoe
ushuhuda kidogo katika kutilia nguvu alichosema Balozi Ramadhani...
Binafsi
(Kalezi Hemedi) na haya ni ya kweli na Allah anashuhudia na wala si kutafuta
fakhari...
Mwaka 2008 nilijiunga na Chuo Kikuu Mzumbe, nilikaa wiki mbili
bila kufanya usajili kwa kuwa Uongozi wa Chuo walitoa sharti la kila mwanafunzi
alipe nusu ya ada ndiyo aweze kusajiliwa.
Kwa
kuwa tulijua kuwa HESLB wangetoa majina ya Wanafunzi waliopata Mkopo mapema, na
kwa kuwa tulijua tuna dhamana ya mkopo wengi katika wanafunzi tulitumai
tusingepoteza nafasi za masomo kwa kutotimiza sharti la chuo
Ajabu,
wale wanafunzi ambao wazazi wao waliweza kulipa nusu ya ada walisajiliwa na Bodi
ya Mikopo walikuwa na utaratibu wa release majina ya wanafaika wa mikopo punde
tu baada ya kupata uthibitisho kutoka vyuoni kuwa wanafunzi husika
walikamilisha usajili.
Hapo
ili nilazimu nirudi Dar nikamuone mshauri wangu mkubwa wa masuala yangu ya
maisha (Marehemu Sheikh Idd Hussein Nyamweru Ndola wa Mwananyamala) ambae
baadae aliniridhia nimuoe bint yake na kuwa mkwe wangu.
Nilivyofika
kwa Sheikh Idd nikamuhadithia na akaingia ndani akanipa shs. laki moja, kisha
akanambia... ''Nenda Bandarini, katika Kampuni ya Fast Ferries kamtafute mtu
anaitwa Kassim Kombo, ukimuona mhadithie majambo yako halafu mwambie nimeagizwa
na Sheikh Idd nije nikueleze haya.''
Ada
kwa fani niliyokuwa nachukua kama sikosei ilikuwa ni Tshs 800,000/= kipindi
hicho, na nusu yake ilikuwa ni Tshs 400,000/= kwa hiyo ile laki alonipa Sheikh
Idd ilikuwa haitoshi.
Baada
ya kumueleza Sheikh Kassim Kombo haja yangu, alifurahi na kunipa nasaha nyingi,
akaendelea..."Kwa uharaka wa jambo lako... ntakuelekeza sehemu mbili... hii moja naamini watakuwa na maswali mengi sana na huenda wasikusaidie ila hii
nyingine naamini kwa msaada wa Allah patapatikana faraja ila vyovyote vile
iwavyo akikuuliza nani kakuelekeza... jitahidi usinitaje." Mwisho wa
kumnukuu.
Moja
ni taasisi na siwezi itaja, nilikwenda na yaliyotokea ni kama yalivyoelezwa na
Sheikh Kassim Kombo na mahala pengine ndio kwa huyu mzee wetu Sheikh Islam.
Alhamdulillah,
nilifika Masjid Maamur, ilikuwa ni wakati wa adhuhr, kwa bahati mbaya
nilichelewa jamaa na kumkosa lakini akapatika kijana mhudumu wa Msikiti
akanipeleka, nikakutana nae na kumueleza haja yangu.
Allah Akbar Allahu Akbar, huyu mzee alikuwa mtu, sijui nimuelezeje, ''any way,'' alinambia niende kesho yake na nilifanya hivyo, na akanipa shs. 300,000/=
nikarudi chuo na kuendelea na masomo.
Kwa
ambao tulikuwa Mzumbe miaka ile mtakumbuka kuna kijana wa Mzumbe Secondary, alikuwa
ni yatima na alipata maradhi ya nyonga, sie kipindi tunashtakiwa tatizo lake
kama Viongozi wa Waislam tulichangishana lakini fedha iliyopatikana haikutosha
(nadhani Brother Hashim Majaba unamkumbuka).
Basi
kwa wajihi niliomuona nao Mzee Islam nilipata nguvu ya kumpeleka yule kijana,
lakini kama binadamu niliishia kwenye njia ya mlango wa kuingilia mtaa wake na
kumwelekeza aende nami asinitaje.
Alhamdulillah
alikwenda, na si tu alimsaidia bali alimtafutia Dr. Bingwa wa Muhimbili na
akampeleka na Mzee Issa akawa anasimamia matibabu yake.
Yule
kijana sijui sasa hivi yupo wapi ila alifaulu kusomea Uhandisi katika Chuo Kikuu
cha Dar es salaam....
Jambo
la ajabu ambalo nilikuwa nikiliona kwa yule mzee, maana nyumbani kwake nilikuwa
naenda mara kwa mara kumsalimia... ni Upanga tena Dar, jiko lipo karibu na
sebule kiasi ukiingia nyumbani kwake unaanza jikoni lakini sebule haina joto,
halafu kuna harufu nzuri sana, sana, sana, kiasi nilikuwa naamini huenda pailikuwa
pakiwashwa ubani lakini ule wa ajabu.
اللهم قدس روحه و
ضريحه برضوان
الَّلهُمَّ بَدِّلْهُ دَارًا خَيْرًا من
دَارِهِ وَ اَهلاً خيرا مِنْ اَهْلِه اٰمِيْن
No comments:
Post a Comment