Sunday 11 January 2015

Kumbukumbu ya Miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar:

http://www.mohammedsaid.com/2015/01/skh-ali-muhsin-barwan.html 

Kipindi Maalum Cha Mapinduzi ya Zanzibar
Radio Kheri

Kumbukumbu ya Miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar
Sheikh Ali Muhsin Al – Barwani 1919 – 2006

Msomi , Mwanasiasa, Mshairi, Mhariri wa Gazeti, Mwandishi wa Vitabu, Mwalimu na Mfasiri wa Qur’an Tukufu

Sheikh Ali Muhsin Barwani
Sheikh Ali Muhsin Barwani wakati wa kupigania uhuru wa Zanzibar alikuwa kiongozi wa Zanzibar Nationalist Party (ZNP) vilevile chama hiki kikijulikana kama Hizbu. Kwa mapenzi makubwa wanachama wa Hizbu walikuwa wanamwita, “Zaim,” yaani ''Kiongozi.'' Sheikh Ali Muhsin alipigania uhuru wa Zanzibar mpaka ukapatikana tarehe 10 December 1963. Sheikh Ali Muhsin alishiriki katika mkutano wa katiba Lancaster House. Baada ya mapinduzi yaliyotokea Zanzibar tarehe 12 Januari 1964 Sheikh Ali Muhsin alikamatwa na kusafirishwa Tanganyika ambako alifungwa Ukonga na jela nyingine kwa kipindi cha miaka 10 na miezi michache. Katika kipindi alichokuwa kifungoni Sheikh Ali Muhsin aliandika miswada kadhaa ambayo alikuja kuichapa kama vitabu.Kabla hajafa mwaka 2006 Sheikh Ali Muhsin aliandika kitabu cha maisha yake ambayo ni kumbukumbu ya yote yaliyopitika Zanzibar kabla na baada ya mapinduzi. Baada ya kuachiwa kutoka kifungoni mwaka 1974 Sheikh Ali Muhsin baada ya kuona kuwa hatoweza kuondoka nchini kwa kuwa alinyimwa pasi ya kusafiria, Sheikh Ali Muhsin alitoroka nchini na kukimbilia Kenya ambako kwa msaada wa UNHCR aliweza kusafiri kwenda Cairo.

Hassan Abdallah Khamis Akiendesha Kipindi Cha Kumbukumbu ya Mapinduzi
ya Zanzibar Akimhoji Mwandishi

Mwandishi na Sheikh Ali Muhsin Barwani, Mascut Oman 1999
Mwanamapinduzi Akimvuta Ndevu, "Muarabu."
Mwanamapinduzi Katika Kofia ya Chuma na Mkononi Ameshika Panga

Mwandishi Akifanya Kipindi Cha Kumbukumbu ya Mapinduzi ya Zanzibar
Akisoma Kutoka Kitabu Alichoandika Sheikh Ali Muhsin Barwani
''Kujenga na Kubomolewa Zanzibar''

Bonyeza Hapo Chini Kukisikiliza Kipindi





1 comment:

Unknown said...

ASALAM ALAYKUM!

Mwenye kutaka kujua ukweli upo wapi ni kuangalia na kuyasikiliza yanasomewa na pande mbili tafauti, kisha nikuyapima yale ambayo ameyasikia na kuyasoma na kuja na uamuzi bila ya kufwata mkumbo.

Katika wanaoyapima ya pande mbili mie ni mmoja wapo kwahio nasubiri, hio Audio niendelee kujifunza.